MwanzoBTC / CAD • Sarafu ya dijitali
add
Bitcoin (BTC / CAD)
Bei iliyotangulia
91,649.89
Kwenye habari
Habari kuhusu Soko
Kwenye habari
Kwenye habari
Kwenye habari
Kuhusu Bitcoin
Sarafu ya Bit ni mfumo wa malipo dijitali ambao unatumiwa na mamilioni ya watu bila msimamizi wa juu kama Benki Kuu ilivyo katika nchi mbalimbali. Sarafu hiyo huweza kutumika kwa kubadilishana na sarafu nyingine, bidhaa au huduma.
Sarafu ya Bit ilianzishwa na mtu asiyejulikana au kikundi cha watu chini ya jina la Satoshi Nakamoto na kutolewa kama programu huria mwaka 2009. Kuanzia Februari 2015, wafanyabiashara zaidi ya 100,000 wanakubali Sarafu ya Bit kama malipo.
Kwa mujibu wa utafiti wa Chuo Kikuu cha Cambridge wa mwaka 2017, kuna watu kati ya milioni 2.9 hadi 5.8 wanaotumia malipo dijitali na wengi wao wanatumia sarafu ya bit.
Mara nyingi sarafu ya bit inaitwa "pesa ya dijitali" lakini wataalamu wengi huiona si pesa bali bidhaa ya bahatisho. Paul Krugmann pamoja na wapokeaji wengine wa Tuzo ya Nobel ya Elimu ya Uchumi aliita udanganyifu.
Historia ya Bitcoin ilianza na karatasi nyeupe iliyochapishwa na Nakamoto ikizungumzia namna mfumo huu na sarafu hii inavyofanya kazi mnamo Oktoba 2008, ambayo ilielezea dhana ya sarafu ya kidijitali iliyosambazwa, ambayo inaweza kutumiwa kwa malipo salama na ya moja kwa moja bila ya kuwepo kwa taasisi za kati kama benki. WikipediaKuhusu Dola ya Canada
Dola ya Kanada ni sarafu ya Kanada. Inafupishwa kwa alama ya dola $. Hakuna muundo wa kawaida wa kutofautisha, lakini vifupisho kama Can$, CA$, na C$ hutumiwa mara kwa mara kutofautisha na sarafu nyingine zinazotumia dola. Inagawanywa katika senti 100. Wikipedia