MwanzoNGN / USD • Sarafu
add
NGN / USD
Bei iliyotangulia
0.00062
Habari za soko
Kuhusu Naira
Naira ni sarafu rasmi ya Nigeria na inadhibitiwa na Benki Kuu ya Nigeria. Naira ilianza kutumika rasmi tarehe 1 Januari 1973, ikichukua nafasi ya pauni ya Nigeria, na hivyo kuwa sarafu ya kwanza ya desimali katika historia ya nchi hiyo. Alama ya sarafu ni "₦", na imegawanyika katika vitengo vidogo vinavyojulikana kama kobo. WikipediaKuhusu Dola ya Marekani
Dola ya Marekani ni sarafu rasmi ya Marekani, iliyoanzishwa mwaka 1792 na kutolewa na Hifadhi ya Shirikisho. Ni sarafu kuu ya akiba duniani, inayotumika sana katika biashara ya kimataifa, bidhaa, na masoko ya fedha za kigeni. Mbali na Marekani, nchi kama Ecuador, El Salvador, na Zimbabwe pia hutumia dola ya Marekani kama sarafu yao rasmi.
Dola ya Marekani inapatikana kwa noti za dola 1, 2, 5, 10, 20, 50 na 100. Kuna pia sarafu ya dola 1.
Dola moja ina senti 100. Senti huitwa pia "penny" nchini Marekani. Kuna sarafu za nusu dolar, robo dolar na sarafu za senti 10, 5 na 1.
Hadi mwaka 1969 noti ya dolar ya Marekani ilikuwa na ahadi ya kwamba serikali ya Marekani itampatia kila mtu dhahabu kulingana na thamani ya dola hizi akipenda kuzibadilisha.
Usawa huu na thamani ya dhahabu ulifutwa. Leo hii dola ya Marekani ni pesa ya kuiamini serikali kama pesa zote. Maana yake watumiaji husadiki ya kwamba serikali haitachapisha dola kushinda uwezo wa uchumi na thamani ya bidhaa zilizopo nchini Tanzania.
Tangu mwisho wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia dola ya Marekani imekuwa pesa kuu duniani na sehemu kubwa ya biashara ya kimataifa hukadiriwa kwa dola hizo. Wikipedia